Deuteronomy 5:27-31

27 aSogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mwenyezi Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mwenyezi Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”

28 b Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri. 29 cLaiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!

30 d“Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao. 31 eLakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”

Copyright information for SwhKC